JAMAA AJIUA KWA SUMU YA PANYA KISA MKE WAKE KAGOMA KURUDI

Mfano wa chupa zenye sumu
**

Kijana aliyejulikana kwa jina la Ginasa Petro (30)  mkazi wa kijiji cha Kayenze, kata ya Kafita wilaya ya Nyang'hwale mkoani Geita  amejiua kwa kunywa sumu ya Panya baada ya mke wake Sarah Jeremia kukataa kurudi kuishi naye baada ya hapo awali kuondoka kutokana na mgogoro wa kimapenzi.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Henry Mwaibambe, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba wivu mkubwa ndiyo uliopelekea mwanaume kuchukua maamuzi hayo 

Ameshauri wanandoa  kuwa wanapaswa kuwaona viongozi wao wa dini ili kusuluhisha changamoto zao na si kujitoa uhai.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments