AUAWA KWA KUCHOMA QURAN


Jamaa na wenyeji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa mtu kwa ajili ya mazishi yake huko Khanewal siku ya Jumapili.
****
Mtu mmoja ameuawa na kundi la watu kwa madai ya kuchoma kurasa za Koran katikati mwa Pakistan, Khanewal, polisi wanasema, katika tukio la hivi karibuni la vurugu zinazohusiana na kukufuru ama kukashifu dini nchini humo.

Polisi wanasema zaidi ya watu 80 wamekamatwa kuhusiana na mauaji hayo siku ya Jumamosi katika wilaya ya Khanewal katika mkoa wa Punjab.

Ripoti zinasema kuwa mtu huyo alikuwa chini ya ulinzi wa polisi kabla ya umati wa watu kumteka na kumuua kwa kipigo.

Mwili wake ulikabidhiwa kwa familia yake na mazishi yaliyofanyika siku ya Jumapili.

Waziri Mkuu wa Pakistan Imran Khan amesema suala hilo "litashughulikiwa kikamilifu kwa mujibu wa sheria" na kuomba ripoti juu ya maafisa wa polisi wanaotuhumiwa kwa kushindwa kutekeleza wajibu wao wa kumwokoa mtu huyo.

Munawar Gujjar, mkuu wa kituo cha polisi mjini Tulamba, ambako tukio hilo lilitokea, aliliambia shirika la habari la AP kwamba mwathiriwa huyo "alikuwa na matatizo ya akili kwa miaka 15 iliyopita".

Chanzo - BBC Swahili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments