HILI NDIYO ZIWA LENYE MAJI YA PINKI




UNAAMBIWA haya ni maajabu ya dunia, nchini Australia kuna maziwa na mito yenye muonekano tofauti na ilivyozoeleka ambapo Ziwa hili la Hillier ni maarufu kutokana na maji yake kuwa ya rangi ya pink.

Ziwa hilo lipo kwenye Visiwa vya Recherche vilivyopo Australia Magharibi likiwa pembeni kabisa mwa bahari ya Hindi, na ukanda wa msitu wa kijani kibichi unaofanya kazi kama kizuizi.

Ziwa hili linasadikiwa kuwa na kiwango cha juu cha chumvi na rangi hii ya pink inatokana na maji ya chumvi kuchanganyika na sodium bicarbonate (baking soda) au vijiumbe hasa mwani unaopenda chumvi (dunaliella salina) na bakteria waridi (halobacteria) ambao huhusaindia kuzalisha rangi hiyo.

Hillier lina urefu wa mita 600 (2,000 ft) na upana wa mita 250 (820 ft) na lilizinduliwa mwandishi Matthew Flinders, mnamo Januari 15, 1802 na sasa linaitwa Flinders Peak.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments