WATU WATATU WAFARIKI, 11 KUJERUHIWA AJALI YA BASI DODOMA


Watu watatu wamefariki dunia na wengine 11 kujeruhiwa katika ajali basi iliyotokea katika eneo la Panda Mbili wilayani Kongwa mkoani Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo chanzo chake amesema ni mwendo kasi.

Naye mkuu wa wilaya ya Kongwa amewatahadharisha wakazi wa wilaya hiyo wanaoishi pembezoni mwa barabara kuu kutoa taarifa kwa jeshi la polisi pindi wanapoona ukikwaji wa sheria za barabarani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments