SIMBA SC YATWAA UBINGWA MAPINDUZI CUP


Simba SC imeandika historia mpya baada ya kubeba Kombe la Mapinduzi kwa kuitandika Azam FC kwa goli 1-0 katika uwanja wa Amaan, Zanzibar.
*************

NA EMMANUEL MBATILO

Klabu ya Simba wamefanikiwa kunyakua taji la Mapinduzi Cup mara baada ha kuwachapa Azam Fc kwenye mchezo ambao ulihudhuriwa na Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt.Hussein Ali Mwinyi.
 
Bao pekee la Simba Sc liliwekwa kimyani na Meddie Kagere ambaye alipachika kwa mkwaju wa penati mara baada ya Sakho kuchezewa faulu ndani ya boksi.

Mchezo huo ambao ulikuwa na hisia kwa mashabiki uwanja wa Amani ulijawa na Mashabiki wengi ambao walioshuhudia mtanange huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments