COASTER YAGONGA TRENI DAR, WATU WAWILI WAFARIKI, 11 WAJERUHIWA


UONGOZI wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) umethibitisha kutokea kwa tukio la ajali lililotokea Januari 19, 2022 maeneo ya Banana jijini Dar es Salaam katika kivuko cha reli na barabara, ambapo gari la abiria aina ya ‘Coaster’ lenye namba za usajili T701 CKD linalofanya safari kati ya Tandika na Mbezi limegonga treni.

"Ajali imetokea majira ya saa 11:10 jioni na imehusisha treni ya mjini inayotoa huduma ya usafiri wa abiria kati ya Kamata na Pugu jijini Dar es Salaam, katika ajali hii majeruhi ni abiria 6 waliokuwa wakisafiri na basi ambapo wanawake ni watatu na wanaume watatu na kuna vifo vya wanawake wawili, majeruhi wote wamepelekwa Hospitali ya Amana kupatiwa matibabu.


"Dereva wa basi alitahadharishwa kwa kupigiwa honi na dereva wa treni, hakuzingatia na hata aliposimamishwa na mshika bendera dereva wa basi aliamua kukatiza reli na kupelekea ajali.


"Uongozi wa Shirika la Reli Tanzania unaendelea kusisitiza Umma kuwa makini na kufuata Sheria na taratibu zinazoonesha alama zilizopo katika vivuko vya reli na barabara na dereva anapokaribia makutano anapaswa kupunguza mwendo na kusimama umbali wa mita 100 kuhakikisha endapo njia ni salama ili kuendelea na safari;

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments