TANESCO YATANGAZA MGAWO WA UMEME NCHI NZIMA


Jengo la Shirika la Umeme nchini (TANESCO)
**
SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco) limetangaza rasmi kuanza mgao wa umeme wa siku 12 nchi nzima kuruhusu matengenezi ya mitambo ya kufua umeme kote nchini.


Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco Maharage Chande ametangaza leo Ijumaa Januari 28,2022 kuwa mgao huo utaanza Jumamosi, Januari 29 hadi Februari 10 mwaka huu.

Taarifa na ratiba ya mgao huo itatolewa kuruhusu watanzania na taasisi kupanga ratiba zao. 

Kwa mujibu wa Tanesco maboresho katika mtambo wa kufua umeme wa Kinyerezi I na Ubungo III yataongeza uzalishaji kutoka megawati 150 hadi megawati 335.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments