KIFAA CHA KUSAIDIA WATU KUJIUA CHAZUA UTATA




Mtengenezaji wa kifaa cha kujiua alisema ana uhakika kinaweza kutumika nchini Uswizi kuanzia mwaka ujao.

Sarco iliomba ushauri wa mtaalamu wa sheria, na akaihakikishia kuwa kifaa hicho hakikiuki sheria za Uswizi.

Lakini wanasheria wengine walihoji usahihi wa msimamo wake. Shirika la Dignitas, ambalo linahusika na suala la kusaidiwa kujiua, lilisema hakuna uwezekano kuwa kifaa hicho "kukubalika kwa kiasi kikubwa". Kujiua kwa kusaidiwa ni halali nchini Uswizi. Na watu 1,300 walikufa, kwa njia hiyo mnamo 2020.

Mkanganyiko wa kisheria

Njia inayotumika kwa sasa Uswizi ni kumpa mtu anayetaka kujiua majimaji, yakimeng'enywa maisha yake yataisha.

"Vidonge vya kujiua" vinaweza kuwekwa popote, vimejaa nitrojeni, na hupunguza haraka viwango vya oksijeni. Husababisha mtu kupoteza fahamu, na kisha kufa ndani ya dakika 10.

Kifaa kinaweza kuendeshwa kutoka ndani, na kina kitufe cha dharura cha kusaidia kutoka humo.

Sarco ilimwomba mtaalamu wa sheria Daniel Herlmann, profesa mshiriki katika Chuo Kikuu cha St. Gallen, kuthibitisha ikiwa matumizi ya kifaa cha kujitoa uhai yalikiuka sheria za Uswizi.

Aliambia BBC kuwa alidhani kifaa hicho "si kifaa cha matibabu" na kwa hivyo hakiko chini ya Sheria ya Bidhaa za Tiba.

Pia inaaminika kuwa haikiuki sheria zinazohusiana na matumizi ya nitrojeni, silaha au usalama wa bidhaa. Alihitimisha kuwa "Sheria za Uswizi hazishughulikii kifaa hiki."

"Uswizi imekuwa na sera ya kusaidiwa kujiua kwa miaka 35," Dignitas aliambia BBC. "Kwa kuzingatia matendo haya ya kitaalamu hatuwezi kufikiria kuwa kifaa cha kuokoa maisha kinaweza kukubaliwa au kuvutiwa na Uswizi."

CHANZO - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments