DKT. GWAJIMA AFANYA ZIARA YA KUKAGUA MAENDELEO YA JENGO LA HOSPITALI YA SEKOU-TOURE


Na WAMJW- Mwanza

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima amefanya ziara ya kukagua Maendeleo ya jengo la mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza- Sekou-Toure.

Katika ziara hiyo ameagiza kasi iendelee katika kukamilisha mradi huo ambao sasa uko asilimia 88 na huduma za uzazi zianze kutolewa katika jengo hilo kabla ya Januari, 2022 kama Mkandarasi alivyoahidi.

Dkt. Gwajima ameelekeza kuanzishwe daftari la kuandika taarifa ya kilichotekelezwa Kila siku ili kuweza kuongeza kasi na kujua kila hatua katika mradi huo ili kuongeza uwajibikaji.

Katika ziara hiyo Dkt. Gwajima aliambatana na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Thomas Lutachunzibwa.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments