Tanzia : NGULI WA PICHA TANZANIA RAMADHANI TONGE AFARIKI DUNIA




Mzee Ramadhani Tonge ambaye aliwahi kuwa mkufunzi wa masuala ya picha katika vyuo vya uandishi wa habari jijini Dar es Salaam amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Amana, Ilala  Jijini  Dar es Salaam na mwili wake utasafirishwa kwenda Morogoro kwa ajili ya mazishi.

Kwa nyakati tofauti, Mzee Tonge alitoa huduma ya ukufunzi katika Chuo cha Uandishi wa Habari cha Times School of Journalism (TSJ) cha Ilala Shariff Shamba jijini Dar es Salaam.

Pia aliwahi kuwa mkufunzi Dar es Salaam School of Journalism kilichopo Ilala, Sharrif Shamba na kuhudumu SHIHATA, Idara ya Habari MAELEZO na kwingineko kama mpiga picha.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments