WAZIRI MKUU AONGOZA MAZISHI YA OLE NASHA






ALIYEKUWA Naibu Waziri wa Uwekezaji na Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro William Tate Ole Nasha amezikwa jana Oktoba 02 2021 katika kijiji cha Osnoni Wilaya ya Ngorongoro

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria mazishi hayo ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,Spika wa Bunge Job Ndugai,Katibu wa Siasa na Itikadi wa Chama cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka ,Mawaziri na Manaibu Mawaziri,pamoja na Wabunge.

Majaliwa ambaye ameshiriki katika mazishi hayo kwa niaba ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amesema kifo cha Ole Nasha ni pigo kubwa kwa Serikali, Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bunge pamoja na kwa wanafamilia na wananchi wa Ngorongoro



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments