Rais Samia Amedhamiria Kumshusha Mama Ndoo Kichwani – Majaliwa
Thursday, October 07, 2021
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Meneja wa RUWASA Wilaya ya Kilwa, kufanya utafiti wa kina wa maeneo ambayo yatawezesha upatikanaji wa maji safi na salama katika maeneo yote yenye changamoto ya maji katika wilaya hiyo.
Amesema Serikali inayoongozwa na mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuhakikisha huduma ya maji safi na salama inapatikana katika kila kijiji ikiwa ni utekelezaji wa kampeni yake ya kumtua mama ndoo kichwani.
Ametoa maagizo hayo jana (Jumatano Oktoba 6, 2021) wakati akizungumza kwa nyakati tofauti na wakazi wa vijiji vya Nasaya, Chumo na Kipatimu akiwa katika ziara ya kikazi ya kukagua miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Lindi.
“Utafiti lazima ufanyike ili tujue wapi tunapa maji, Rais Samia anatoa pesa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi, piteni mpime maeneo yote mtafute vyanzo na mtuambie maji yako kiasi gani, mitambo na wataalam tunao.”
Awali, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Chumo, Waziri Mkuu ametoa onyo kwa wafugaji wenye tabia ya kuingiza mifugo katika mashamba ya wakulima. “Viongozi wekeni utaratibu wa kukutana na wafugaji na kuwaelimisha ili wafuge kulingana na ukubwa wa maeneo yao.”
Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali inaendelea na mpango wake wa kuunganisha mtandao wa barabara Wilaya kwa Wilaya baada ya kukamilika kwa mpango wa kuunganisha makao makuu ya mikoa kwa barabara za lami.
“Meneja wa TANROADS nimeona ukarabati unaoendelea hakikisha barabara hii inafanyiwa ukarabati wa mara kwa mara na iwe inapitika kipindi chote.”
Akiwa katika kijiji cha Miteja Waziri Mkuu alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Zainab Kawawa asimamia ujenzi wa Kituo Shikizi cha Masaninga ambacho kimejengwa kwa nguvu ya wananchi hadi kufikia hatua ya upauaji.
Amesema hadi kufikia tarehe 4 ya mwezi Novemba shule hiyo iwe imekamilika na kuchangia shilingi milioni tano ikiwa ni hatua ya kuunga mkono jitihada za wananchi wa kijiji hicho.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu alitembelea kiwanda cha kusindika vinywaji cha Hopaje kilichopo Nangurukuru Wilayani Kilwa, ambapo amesema Mheshimiwa Rais Samia ameendelea na utekelezaji wa sera ya viwanda na kuvutia wawekezaji ili kukuza uchumi kwa kuweka mazingira bora ya uwekezaji.
(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin