MIONGOZO ADA ZA UKUSANYAJI TOZO ZA UMWAGILIAJI WAKAMILIKA



Kaimu Mkurugenzi Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali akizungumza na waandishi wa Habari Ofisini kwake jijini Dodoma kuhusiana na uchangiaji wa Tozo katika sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji.
**


Na Mwandishi Wetu – Dodoma
Katika kutekeleza agizo la Serikali linalowataka wakulima wote wanaojishughulisha na shughuli za kilimo cha umwagiliaji kuachangia asilimia tano katika mfuko wa maendeleo ya kilimo cha Umwagiliaji, Tume ya taifa ya Umwagiliaji imekamilisha Miongozo kanuni na taratibu za ukusanyaji wa tozo za Kilimo cha Umwagiliaji.

Hayo yamesemwa Mapema Leo jijini Dodoma na Kaimu Mkurugenzi mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake.

Bw. Kaali alisema mapema mwezi July Mwaka huu Serikali kupitia Waziri wa Fedha ilitoa agizo ya wakulima waliyopo katika skimu za kilimo cha umwagiliaji kuchangia asilimia tano kwa kila hekta na fedha hizi ziingizwe katika mfuko wa umwagiliaji kwa ajili ya kugharamia matunzo, matengenezo pamoja na uendeshaji wa skimu za kilimo cha umwagiliaji.

Aidha Mkurugenzi Kaali amesema kuanzia mwezi huu wa kumi Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inaanza kampeni maalum ya kutoa elimu kuhamasisha wananchi mbali mbali wachangie watoe hizi ada kwa ajili a kuendeleza kilimo cha umwagiliaji, “Hivyo watumishi mbalimbali kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na viongozi mbali mbali wa serikali watakwenda katika maeneo mbalimbali ya nchi,kwa ajili ya kuelemisha na kuhamasisha utoaji wa ada hizi za umwagiliaji.” Alisema Kaali

Bw. Kaali wamewaasa wakulima wanaojihusisha na kilimo cha Umwgiliaji kuchangia ada za umwagiliji kwani amesema ni fursa nzuri ssaa ambayo imetolewa na Serikali kuchangia fedha katika mfuko wa umwagiliaji ili kuweza kutatua changamoto kubwa katika skimu mbalimbali hapa nchini.

Kwa pande wake Kaimu Mkurugenzi uendeshaji Bwana Enterbet Nyoni amesema katika skimu za kilimo cha umwagiliaji zisozendelezwa mgawanyo wa Ada ya tozo ya asilimia tano ya tozo, utahusisha asilimia sabini na tano (75%) kubakia katika skimu husika na asilimia ishirini na tano (25%) itakwenda katika mfuko wa maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post