DKT. MAHENGE: TUTATUMIA KILA MBINU WANANCHI WAPATE CHANJO YA UVIKO 19 SINGIDA

Mkuu wa Mkoa Singida Dkt.Binilith Mahenge akizungumza kwenye kikao cha kamati ya afya ya msingi ya jamii  (PHC) Mkoa wa Singida kilicho keti leo kuhusu utekelezaji wa mpango shirikishi na harakishi kwa ajili ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Singida Alhaj Juma Kilimba na Mganga Mkuu Mkoa wa Singida Victorina Ludovick.
Mganga Mkuu Mkoa wa Singida Victorina Ludovick akizungumza kwenye kikao hicho.
Katibu Tawala Mkoa wa Singida Dorothy Mwaluko akizungumza kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Mwakilishi kutoka Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali ya Mitaa (TAMISEMI) Idara ya Jamii  na Lishe, Dinah Atinda (kulia) na Richard Magodi kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto wakiwa kwenye kikao hicho. 

Viongozi wa dini wakiwa kwenye kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Mratibu wa Health Promotion Mkoa wa Singida, Habibu Mwinory akichangia jambo kwenye kikao hicho.
            Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili akichangia jambo kwenye kikao

          Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo akichangia jambo kwenye kikao

Mwakilishi kutoka Shirika la Sema na Mjumbe wa Taifa wa Baraza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Singida Peter Lissu akichangia jambo kwenye kikao hicho.
Mratibu wa TASAF Mkoa wa Singida, Patrick Kasango akichangia jambo kwenye kikao hicho.
    Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Joseph Kyense akichangia jambo kwenye kikao hicho

 


Na Dotto Mwaibale, Singida


MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt.Binilith Mahenge amesema watatumia kila mbinu ili kuona wananchi wa mkoa huo wanapata chanjo ya Uviko-19.

Dkt.Mahenge ameyasema hayo leo kwenye kikao cha kamati ya afya ya msingi ya jamii  (PHC) Mkoa wa Singida kilicho keti kuhusu utekelezaji wa mpango shirikishi na harakishi kwa ajili ya utoaji wa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Uviko 19.

"Tumekwisha anza kuona matokeo mazuri ya watu kujitokeza kupata chanjo, hii inatokana na kazi nzuri na mbinu mbalimbali za uhamasishaji naomba tusimame hapo na twende tukaeneze hizo juhudi ninachohitaji ni kuona watanzania wengi wanapata chanjo,". alisema Mahenge.

Alisema zitatumika kila mbinu katika kukamilisha kazi hiyo kwani kwenye msafara wa mamba kenge hawakosekani hivyo ni wajibu wetu tufanye kila liwezekanalo ili wabaki mamba na kuachana na hao kenge ambao wanazohofisha jitihada hizo.

Alisema kazi hiyo inawezekana hasa baada ya hizi siku chache kuongezeka kwa idadi ya wananchi kujitokeza kupata chanjo hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo alisema muitikio wa wananchi kupata chanjo hiyo ni mkubwa zaidi maeneo ya vijiji tofauti na mijini ambapo alitolea mfano wa Singida Mjini ambayo imepitwa na Singida Vijijini hivyo akaomba uhamasishaji katika maeneo ya mijini uongezewe nguvu.

Mchungaji wa Kanisa la Anglikana Joseph Kyense aliiomba Serikali iendelee kuleta chanjo nyingi zaidi ili kila mwananchi aweze kuchagua chanzo atakayoipenda badala ya kuwa na moja tu.

Mkuu wa Wilaya ya Singida Mhandisi Paskas Muragili alisema kupitia mpango huo Shirikishi na Harakishi wananchi wamekuwa na muitikio hasa baada ya kueleweshwa umuhimu wa chanjo hiyo.

 Mwakilishi kutoka Shirika la Sema na Mjumbe wa Taifa wa Baraza la Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Singida Peter Lissu alisema kesho kwa kushirikiana na Civil Society Foundation watakuwa na kikao na Mashirika 50 ya mkoani hapa kwa ajili ya kuona mchango wao wa uhamasishaji wananchi kujitokeza kupata chanjo hiyo.

Mwenyekiti wa Dini mbalimbali Mkoa wa Singida Sheikh Hamisi Kisuke alisema zoezi la kwenda kuhamasisha nyumba kwa nyumba ili watu wajitokeze kupata chanjo  limefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwa kuongeza idadi ya watu tofauti na mwanzo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments