WANAWAKE WAANDAMANA KUPINGA KUZUIWA KUTOA MIMBA



Maelfu ya wanawake wameandamana katika miji kadhaa nchini Marekani kupinga kampeni ya kihafidhina inayolenga kudhibiti au kuzuia huduma za kutoa mimba.

Mjini Washington, takriban waandamanaji 10,000 walijitokeza karibu na ikulu (White House), kabla ya kuelekea katika majengo ya mahakama ya juu ambayo itatoa uamuzi wa mwisho kuhusu suala hilo lenye utata.

Waandamanaji walibeba mabango yenye maneno kama, Halalisha uavyaji mimba na pia mwili wangu, chaguo langu.

Suala hilo limekuwa tete zaidi tangu Septemba mosi wakati jimbo la Texas lilipopitisha sheria ya kupiga marufuku utoaji wa mimba, hatua iliyoanzisha upinzani mkali bungeni.

Siku mbili tu kabla ya mahakama ya juu kuanza kushughulikia kesi hiyo, kumekuwa na maandamano katika zaidi miji 600.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments