Post Top Ad
Monday, October 11, 2021
MWANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE AUAWA KWA KUCHOMWA AKIGOMBANIA MWANAMKE BAA
Mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya upili ya Kapsinendet kaunti ya Bomet nchini Kenya amefariki dunia baada ya kudungwa kisu na mwanaume mmoja wakiwa kwenye baa wakigombania mwanamke.
Inaelezwa kwamba wawili hao walikuwa wakizozania mwanamke mmoja kwenye baa kabla ya mshukiwa kuchukua kisu na kumdunga mwanafunzi huyo.
Kwa mujibu wa taarifa za Citizen, mwanaume huyo ambaye hajatambulika anadaiwa kumdunga mwathiriwa kisu mara mbili kwenye shingo kabla ya kutoroka.
Mwanamke aliyekuwa akipiganiwa alitoroka eneo la tukio baada ya kushindwa kuwatuliza wanaume hao
Mwanamke huyo anasemekana alihamia eneo la Siongiroi kutoka Sotik hivi karibuni.
Maafisa wa polisi walifanikiwa kumkamaata mshukiwa na wanamzuilia katika kituo cha Chebunyo kaunti ya Bomet huku uchunguzi ukianzishwa.
Chanzo - Tuko News
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post Top Ad
Author Details
Malunde 1 blog ni blog ya Kiswahili maarufu duniani kwa habari za Matukio, Siasa, Magazeti, Nyimbo za asili na habari za kusisimua.
No comments:
Post a Comment