KESI YA MBOWE: MSHTAKIWA ADAI HAKUPEWA CHAKULA KWA SIKU 10


Shahidi wa pili upande wa utetezi katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi inayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake, Mohamed Ling’wenya amedai hakula chakula siku kumi akiwa katika kituo cha polisi Mbweni.

Shahidi huyo amedai alifikishwa kituo cha polisi Mbweni Agosti 9, 2020 hadi Agosti 19, 2020 alipofikishwa mahakama ya Kisutu ndipo alikula ugali na dagaa.

Ling’wenya ametoa madai yake leo Jumanne Septemba 28, 2021 katika mahakama kuu divisheni ya makosa ya rushwa na uhujumu uchumi wakati akitoa ushahidi wake katika kesi hiyo ndogo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments