DAKTARI AWAUA WATOTO WAKE WAWILI KWA KUWACHOMA SINDANO




DAKTARI mmoja katika eneo la Nakuru nchini Kenya anadaiwa kuwaua wanawe wawili wenye umri wa miaka mitano na mitatu kwa kuwachoma sindano.

Dk. James Gakara alikutwa amelala kando ya wanawe akiwa amepoteza fahamu katika kisa ambacho anashukiwa kutekeleza mauaji na kujaribu kujiua.

Dk. Gakara ambaye alikimbizwa ili kupata matibabu katika Hospitali ya Nakuru Level Five, naye aliaga dunia Jumatano, Septemba 22, 2021.

Kulingana na ripoti ya upasuaji wa maiti, Gakara alimeza kemikali isiyojulikana ambayo huenda ilisababisha kifo chake.

Daktari aliyeendesha zoezi la upasuaji kubaini chanzo chake, Dkt. Titus Ngulungu amesema kwamba huenda marehemu alikunywa dawa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments