BETWAY YATANGAZA KUINGIA TANZANIA


Hadhara Charles, mtaalamu wa kuchezea mpira akionesha ufundi wake wakati wa tukio la utambulisho wa kampuni ya Betway Tanzania. Uzinduzi umefanyika Agosti 11, 2021 jijini Dar es Salaam.

11 Agosti 2021 - Dar es salaam
Betway, kampuni ya kimataifa ya michezo ya kubashiri, wameingia rasmi katika soko la Tanzania. Lengo la kampuni hiyo ni kutoa huduma bora, za kipekee na rahisi kwa wapenzi wa michezo ya kubashiri nchini Tanzania ambao wanaweza kubashiri michezo ya ndani na ya kimataifa. 

Wakati kampuni inaanzishwa mwaka 2006, lengo la Betway lilikuwa ni kuleta ushindani katika tasnia ya michezo ya kubashiri. Kampuni imeendelea kukua mwaka hadi mwaka.

Hii imetuwezesha kuingia kwenye soko la Tanzania tukiwa na michezo mingi, yenye masoko tofauti ya kubashiri, mfumo wetu wa kubashiri Live na eSports ni wa kisasa zaidi. 

Tunajivunia kufanya kazi katika nchi ambazo sekta ya michezo ya kutabiri imeratibiwa, kwa sasa tuna leseni za kufanya kazi katika nchi 12 ikiwa ni pamoja na Kenya, Ghana, Afrika Kusini, Uganda, Zambia, Msumbiji na Nigeria. Tunayo matumaini makubwa kwamba uwekezaji wa kampuni yetu katika soko la Tanzania utapelekea Tanzania kuwa kitovu cha mafanikio ya michezo katika bara la Afrika. 

Katika kuhakikisha tunafikia malengo tuliyojiwekea, tumeweka machaguo mbalimbali ambayo yanakidhi uwezo wa mtanzania wa kawaida. Wateja wanaweza kuweka pesa kwenye akaunti zao na kutoa pesa kwa urahisi na salama kwa kutumia njia mbali mbali za malipo. Kwa kusaidia wateja kuanza safari yao ya kubashiri, mteja mpya atapata Free Bet TSh 3,000 kwa kujisajili.

Kwa niaba ya serikali ya Tanzania, Mkurugenzi wa Idara ya Michezo kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Addo Komba ameikaribisha Betway nchini Tanzania na kuwahakikishia ushirikiano kutoka serikalini na kwa wadau wengine wa michezo.

“Ninafurahi kupewa heshima kuwa mgeni rasmi katika hafla hii muhimu sana ya kuikaribisha Betway nchini Tanzania. Serikali inafurahi kuona wawekezaji wapya kama Betway wanaingia Tanzania kwa nia ya kuunga mkono juhudi za maendeleo katika michezo. Betway ni kampuni kubwa ya michezo ya kubashiri kwa hivyo uamuzi wao wa kuja Tanzania ni ishara nzuri kwetu kwamba tunapiga hatua na wako tayari kutusukuma zaidi”, alisema Komba.

Mbali na kutoa burudani ya kusisimua uwanjani, pia tuna mipango kadhaa ya kusaidia jamii nje ya uwanja. Ni kwa mapenzi yetu ya michezo na nia ya maendeleo ya michezo tunauwezo wa kutoa msaada kwa jamii katika michezo yenye uhitaji. 

Meneja Uendeshaji wa Betway Tanzania, Jimmy Masaoe alisema kwamba;
“Ni wakati mzuri katika sekta ya michezo ya kubashiri na tunaamini kwa uzinduzi wa bidhaa hii yenye ubora wa kimataifa kwenye soko, tunauwezo wa kuleta msisimko kwa wanaobashiri na mashabiki, wakati bado tunarudisha kwa jamii kupitia miradi mbali mbali ya michezo.”

Kama kampuni ya michezo ya kubashiri, ni jukumu letu kuhakikisha tunaweka mazingira rafiki kwaajili ya kubashiri kistaarabu.

Kuhusu Betway Group
Betway Group ni kampuni inayotoa huduma ya daraja la kwanza kwenye michezo ya kubashiri. Ilianzishwa mwaka 2006, kampuni inafanya kazi katika nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda, Ghana, Afrika Kusini, Zambia, Msumbiji, Nigeria na Tanzania.
Betway inajivunia kuwapa wateja wake huduma bora za kubashiri, kuwaburudisha, kuwapa taarifa pamoja na kuhakikisha wanashiriki michezo ya kubashiri katika mazingira salama.
Kwa maelezo zaidi kuhusu Betway tembelea: www.betway.co.tz

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments