WAZIRI SIMBACHAWENE ARUHUSU KUTUMIKA KWA NYUMBA ZA ASKARI
Saturday, July 10, 2021
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi George Simbachawene ameruhusu askari polisi kuanza kutumia nyumba za kisasa zenye uwezo wa kukaliwa na familia zaidi ya 300 zilizopo eneo la Kunduchi na Mikocheni mkoani Dar es salaam.
Waziri Simbachawene amesema hayo wakati wa ziara yake ya kukagua mradi huo wa nyumba za kisasa za makazi ya askari.
Amesema kuanza kutumika kwa nyumba hizo kutasaidia kupunguza uhaba wa nyumba za askari, na kutaleta ufanisi kwa askari wanapotekeleza majukumu yao ya kazi za Kipolisi.
Kwa upande wake mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro amesema zaidi ya miaka mitatu imepita tangu kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa nyumba hizo.
Amesema baadhi ya nyumba hizo kwa sasa zimeanza kuchakaa kutokana na kutokaliwa kwa muda mrefu, pamoja na kukosa matunzo.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin