RAIS YOWERI MUSEVENI AAGIZA WANAOSAMBAZA UVUMI KUWA AMEFARIKI WAKAMATWE

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema kuna haja ya kuwakamata raia wa taifa hilo wanaotumia mitandao ya kijamii vibaya.

Akizungumza na vyombo vya habari rais huyo ameshutumu wale wanaosambaza habari kwenye mitandao kwamba yeye amefariki dunia.

Amesema kwamba wale wanaohusika na habari kama hizo wanapaswa kusakwa na kukamatwa kwa kuwa wamekuwa wakipotezea watu muda wao.

Alisema: Tatizo jingine ambalo linapaswa kutatutiliwa ambalo sio la kiusalama bali la kijinga ni mitandao ya kijami. Mitandao ya kijami imekuwa ikisema kwamba museveni amefariki. Hivyobasi naitaka idara ya usalama kusuluhisha tatizo hilo.

Social embed from twitter


Nataka wawafuatilie kwa haraka wale wanaozua uvumi kama huo.

Twitter Kumekuwa na uvumi katika siku za hivi karibuni kwamba kiongozi huyo alikuwa amesafirishwa kutoka nchini Uganda na kupelekwa nchini Ujerumani akiwa katika hali mahututi baada ya kuugua maradhi ya tatizo la kupumua linalohusishwa na ugonjwa wa corona.

Hata hivyo akizungumza Rais Museveni alisema kwamba wale wanaozua habari kama hizo wanapaswa kufuatiliwa na vyombo vya usalama ili kukamatwa haraka iwezekanavyo.

Chanzo - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments