Picha : MWANAFUNZI AZUA GUMZO KWA KUVAA MABANGO MWILI MZIMA SHINYANGA MJINI

Mwanafunzi Josephat John, aliyekuwa anasoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kom iliyopo Manispaa ya Shinyanga, amezua taharuki ya aina yake leo mchana Ijumaa Juni 4,2021 mjini Shinyanga mara baada ya kujianika juani huku akiwa amevaa mabango na kujifunika maboksi yenye ujumbe wa kupinga kuchaguliwa masomo ya Economics, Commerce , Accounts (ECA) ambayo amedai hawajawahi kuyasomea kwani yeye amesomea masomo ya Physics, Chemistry, Biology (PCB).

Ametumia mbinu hiyo  ya kuvaa mabango kuiomba Wizara husika ifanye uchaguzi upya wa michepuo ili akasomee masomo ambayo ameshayasoma.

Tukio hili limekuja ikiwa ni siku chache zimepita tangu Waziri wa TAMISEMI Ummy Mwalimu atangaze matokeo ya wanafunzi waliochaguliwa kwenda vyuo vya ufundi na vyuo vya kati na kidato cha Tano mwaka 2021. 

Mwanafunzi Josephat John, aliyekuwa anasoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari Kom iliyopo Manispaa ya Shinyanga, akiwa amevaa mabango na kujifunika maboksi yenye ujumbe wa kupinga kuchaguliwa masomo ya Economics, Commerce , Accounts (ECA) ambayo amedai hawajawahi kuyasomea kwani yeye amesomea masomo ya Physics, Chemistry, Biology (PCB). Picha na Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments