KADA WA CHADEMA MDUDE NYAGALI AACHIWA HURU

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya imemuachia huru kada wa Chadema, Mdude Nyagali aliyekuwa akikabiliwa na kesi ya kukutwa na dawa za kulevya baada ya mahakama kueleza kuwa ushahidi uliotolewa dhidi yake ni batili.
 
Juni 14, 2021, Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya iliahirisha kutoa hukumu dhidi ya kesi yake kwa kile kilichoelezwa kuwa hukumu bado haijakamilika pamoja na mambo mengine ambayo yalikuwa nje ya uwezo wa Hakimu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments