TIGO WAPANDA MITI 500 KUADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA

 

Mkurugenzi wa Tigo, Simon Karikari akipanda miti katika viwanja vya Half London, Hai, Kilimanjaro Tunaadhimisha Maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yenye kauli mbiu “Kurejesha Mfumo wa Ikolojia” kwa kupitia mkakati wetu wa #TigoGreenForKili tunarejesha mazingira mazuri yanayozunguka Ml. Kilimanjaro kwa kupanda miti 28,000 mwaka huu.

KILIMANJARO YETU: Urithi wetu uko mikononi mwetu, tunapanda miti kuhakikisha theruji ya mlima huu mrefu barani Afrika haipotei kutokana na shughuli na mabadiliko ya tabia nchi.

Jackson Haule- Mwakilishi kutoka NEMC akipanda Mti kama mkakati wa kurejesha mazingira salama mkoa wa Kilimanjaro.

Wafanyakazi wa Kampuni ya Northern Engineering wakipanda Miti kama ishara ya kurejesha hadhi ya Ml Kilimanjaro na kuifanya Kilimanjaro ya kijani ten

Mkurugenzi wa Tigo, Simon Karikari akipanda miti katika viwanja vya Half London, Hai, Kilimanjaro

Tunaadhimisha Maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yenye kauli mbiu “Kurejesha Mfumo wa Ikolojia” kwa kupitia mkakati wetu wa #TigoGreenForKili tunarejesha mazingira mazuri yanayozunguka Ml. Kilimanjaro kwa kupanda miti 28,000 mwaka huu.



HATUNA BUDI “Mabadiliko ya tabia ya nchi na shughuli za kibinadamu yameathiri Mazingira ya Mlima Kilimanjaro hivyo hatuna budi kuchukua tahadhari ndio mana kupitia #TigoGreenForKili tutaweza Kurejesha Mfumo wa Ikologia”.
Asifiwe James - Mkurugenzi @voewofo




LENGO KUU “Dhima ya mwaka huu #SikuYaMazingiraDuniani yenye kauli mbiu Kurejesha Mfumo wa Ikolojia, inaendana na mkakati wetu wenye lengo la kurejesha hadhi ya mlima Mrefu barani Afrika kupitia mkakati wa #TigoGreenForKili kupanda miti 28,000 mwaka huu” Mkurugenzi wa Tigo, Simon Karikari



“Mazingira ni muhimu & ni chanzo cha uhai wetu, hatuna budi kuyatunzq ili yatutunze hasa kupitia mkakati huu ambao @tigo_tanzania wamekuja nao” Jackson Haule- Mwakilishi kutoka NEMC

AHADI YETU KWENU: “Tunawahakikishia kuilinda vyema miti hii 500 tutakayoipanda katika viwanja vya Half London ili kwa pamoja tuweze kuifanya Kilimanjaro iwe ya kijani tena.” Mkurugenzi wa mamlaka ya Mji wa hai, Noel Nnko
Tumeanza rasmi maadhimisho ya siku ya mazingira duniani yenye kauli mbiu “Kurejesha Mfumo wa Ikolojia”. Kupitia mkakati wa #TigoGreenForKili 
tumedhamiria kurejesha mazingira mazuri yanayozunguka Ml. Kilimanjaro kwa kupanda miti 28,000 mwaka huu. Kupitia michango mbalimbali kutoka kwa wadau mbalimbali tumeweza na tunaendelea kupanda miti katika maeneo mbalimbali mkoa wa Kilimanjaro.

.
Tunapongeza & kuwashukuru wadau wetu wote walioitikia wito huu


 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments