WANNE WAFARIKI DUNIA, 20 WAJERUHIWA AJALI YA BASI SHINYANGA, RPC ATAJA MAJINA

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magiligimba, akiangalia bas ambalo limepata ajali ya kuuwa watu Wanne na kujeruhi 20, na kwenye basi hilo kulikuwa na abiria 43.

Na Mwandishi wa Malunde 1 blog, Shinyanga
Watu wanne wamefariki dunia katika ajali ya basi Kampuni ya Classic lenye namba za usajili binafsi Salum Rashidi Classic (SRC 3), likitokea Kampala nchini Uganda kwenda Jijini Dar es salaam.

Ajali hiyo imetokea leo majira ya saa 10 alfajiri katika Kona ya Didia wilayani Shinyanga, na kusababisha vifo vya abiria hao na majeruhi 20, ambapo wanapatiwa matibabu hospitalini.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga ACP Debora Magiligimba, amewataja watu waliofariki katika ajali hiyo kuwa ni Wahida Yusuph mkazi wa Pemba, Joseph Joseph mkazi wa Dar es salaam, Rehema Haji mkazi wa Unguja, na Nasorro Hamisi mkazi wa Zanzibar.

Amewataja majeruhi watano ambao wamekatika viungo vya miili yao, kuwa ni Njama Hassani, Fatuma Kesi, Sada Manga, na Twalibu, wote wamekatika mkono wa kushoto na mmoja mguu wa kulia, pamoja na Mohamed Daudi mkono wa kulia.

Aidha amesema majeruhi wengine 15 walitibiwa na kuruhusiwa, na hali zao zinaendelea vizuri, na kubainisha kuwa basi hilo lilikiwa na abiria 43 ambapo wengine ni wazima hawakuumia.

"Chanzo cha ajali hii ni mwendo kasi, ambapo Dereva wa basi anayejulikana kwa jina la Maxison Mkuru alishindwa kukata Kona na kusababisha ajali, na tunamsaka kwa sababu amekimbia," alisema Magiligimba.

“Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufani mkoani Shinyanga, na majeruhi wanaendelea na matibabu, na ninatoa wito kwa madereva kuzingatia sheria za usalama barabarani,”ameongeza.

Nao baadhi ya abiria waliokuwa kwenye basi hilo akiwamo Fotuna Wilbert, amesema baada ya kufika kwenye kona hiyo ya Didia basi likiwa katika mwendo kasi, walishaghaa kuona linayumba na kumshinda dereva na kupata ajali.

Soma pia : 

BASI LA CLASSIC LAPATA AJALI BUYUBI - SHINYANGA

TAZAMA PICHA ZA AJALI HAPA CHINI
Baadhi ya abiria ambao wamenusurika kwenye ajali ya basi, wakiangalia mizigo yao.
Askali Polisi wakiwa na wafanyakazi wa mgodi wa madini ya dhahabu Buzwagi, wakiangalia namna ya kulinyanyua basi hilo.
Zoezi la kunyanya basi likiendelea.
Basi likiwa limenyanyuliwa.

Picha na Marco Maduhu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments