RAIS SAMIA KUZUNGUMZA NA WAZEE 900 WA DAR KESHO

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kesho Ijumaa Mei 7, 2021 anatarajia kuzungumza na wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika mkutano utakaofanyika ukumbi wa Mlimani City na kuhusisha wazee takribani 900.



Hayo yameelezwa leo Alhamisi Mei 6, 2021 na mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge aliyebainisha kuwa kulikuwa na utaratibu maalum wa kuwapata wazee hao na kwamba wengine wanapaswa kufuatilia mkutano huo kupitia vyombo mbalimbali vya habari.

Kunenge amewaambia waandishi wa habari kuwa, mkutano huo utafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mlimani City kuanzia saa 8 mchana.

Kunenge ametoa wito kwa Wazee waliopata mwaliko wa kushiriki mkutano huo kujitokeza kwa wingi, ili wapate kusikiliza kile ambacho Rais Samia Suluhu Hassan amewaitia.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments