AMUUA MAMA YAKE KWA MAPANGA AKIMTUHUMU KUMROGA

Mkazi wa kijiji cha Guta Wilaya ya Bunda mkoani Mara Grace Chacha (67) amefariki dunia baada ya kukatwa mapanga na mwanaye wa kambo aitwaye Matiku Chacha akidaiwa ni mchawi.

Mtoto wa marehemu Joseph Chacha amesema tukio hilo lilitokea Aprili 22, 2021 saa 4 asubuhi katika kijiji cha Guta.

Ameelez kuw mama huyo anadaiwa kuuawa na kijana huyo aliyekuwa akiishi jirani na Grace na kwamba kabla ya tukio hilo mtuhumiwa huyo anadaiwa kutamka maneno ya vitisho kwa marehemu akimtuhumu kuwa chanzo cha yeye kuwa na maisha magumu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments