Picha : IBADA MAALUM YA MAZISHI YA HAYATI JPM KATIKA UWANJA WA MAGUFULI CHATO MKOANI GEITA


Viongozi mbalimbali wa Serikali, Wabunge, wasanii pamoja na wananchi tayari wamefika katika uwanja wa Magufuli uliopo Chato mkoani Geita tayari kwa ajili ya ibada maalum ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Kutoka Chato mkoani Geita kwenye ibada maalum ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli. Tayari viongozi mbalimbali na wananchi wameshawasili katika uwanja wa Magufuli ambapo shughuli za ibada zitafanyika.


Viongozi mbalimbali wa Serikali, Wabunge, wasanii pamoja na wananchi tayari wamefika katika uwanja wa Magufuli uliopo Chato mkoani Geita tayari kwa ajili ya ibada maalum ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Viongozi mbalimbali,wasanii na wananchi walianza kuingia katika viwanja vya Magufuli kuanzia majira ya saa 11 alfajiri tayari kabisa kushiriki ibada ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Stanslaus Mabula mbunge wa jimbo la Nyamagana ni miongoni mwa wabunge waliofika Chato katika viwanja vya Magufuli kwaajili ya kumshiriki misa maalum ya mazishi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.

Mwili wa Hayati Magufuli umefika katika viwanja vya Magufuli majira ya saa 03;45 asubuhi na kupokelwa kwa Majozi makubwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Wabunge, wasanii pamoja na wananchi waliofika katika uwanja huo wa Magufuli.

Hayati Magufuli anatarajiwa kuzikwa leo wilayani Chato baada ya Ibada maalumu na Salamu mbalimbali kutolewa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments