BABA AJIUA BAADA YA KUUA MKE NA MTOTO KISA WAMEBADILI DINI


Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi
**
Jeshi la Polisi mkoani Kagera linaendelea kuchunguza tukio la vifo vya watu watatu lililotokea Machi 26, 2021, saa 9:00 usiku katika kijiji cha Mayondwe wilayani Muleba.

Katika tukio hilo baba wa familia aliwaua mke wake na mtoto wake mmoja kwa kuwakata sehemu mbalimbali za miili yao na kisha naye kujiua kwa kujinyonga kwa shuka.

Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi ametaja waliopoteza maisha kuwa ni Editha Martin (48) na Sawia Sudi (25) ambao walikatwa kwa panga na mtuhumiwa Sudi Mwamandi (49) ambaye baada ya kufanya mauaji hayo alijinyonga kwa kujitundika juu ya mti kwa kutumia shuka.

Kamanda Malimi amesema kuwa uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi wa kifamilia, uliotokana na mke wa mtuhumiwa Editha Martin na mtoto wake Sawia Sudi kubadilisha dini kutoka Uisilamu na kuwa Wakristu.

"Kitendo hicho inaonekana kilimkasirisha sana baba wa familia, na mama alipoona ugomvi umezidi alihama na kwenda kuishi sehemu nyingine, na siku ya tukio mtuhumiwa huyo alivamia katika nyumba walikohamia na kumkuta mke wake ambaye alimkata kwa panga na wakati akitoa alikutana na binti yake naye akamkata kwa panga na kusababisha vifo vyao papo hapo", amesema.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments