IGP SIRRO AWATAKA WAENDESHA PIKIPIKI KUFUATA SHERIA
Thursday, March 04, 2021
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewaonya na kuwataka vijana wanaoendesha pikipiki maarufu kama bodaboda, kufuata sheria na alama za barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.
IGP Sirro amesema hayo leo akiwa Kiwangwa mkoani Pwani na kuzungumza na baadhi ya wananchi wa eneo hilo wakati akiwa njiani kuelekea mkoani Tanga, ambapo amesema kuwa, karibu asilimia 90 ya vifo nchini vinatokana na ajali za pikipiki.
Hata hivyo, IGP Sirro amewataka wananchi hususan vijana kuacha kujihusisha na uhalifu wa kutumia silaha, wizi wa mifugo na mazao na kuwataka kujihusisha na biashara halali hasa za ujasiriamali.
Akiwa mkoani Tanga, IGP Sirro amefanya ukaguzi wa eneo la uwanja wa mbinu za medani lililopo Mkomazi mkoani humo na kusema kuwa, jitihada kubwa zinaendelea kufanyika ikiwemo kujenga majengo ya kisasa kwa ajili ya kufanya mafunzo ya utayari kwa askari wa Jeshi hilo.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin