AVULIWA UCHUNGAJI TUHUMA ZA KUMPA MIMBA MUUMINI WA KANISA.. 'ASKOFU AELEZA WALIVYOKWENDA GESTI'

Askofu Heryyabwana Majebele
***
Mchungaji msaidizi wa Kanisa la Ufunuo Ushirombo lililopo wilayani Bukombe mkoani Geita, Maliko Elikana amevuliwa wadhifa wa uchungaji na kuwa mumini wa kawaida kwa tuhuma za kumpa mimba muumini wa kanisa hilo.

Akitangaza kumvua uchungaji huo kanisani, Askofu wa Jimbo la Geita la kanisa hilo, Heryyabwana Majebele amesema ana ushahidi wa kutosha na amefuatilia mienendo ya mchungaji huyo na kubaini walikuwa wanakwenda katika nyumba ya kulala wageni na muumini huyo.

Hata hivyo, Mchungaji Elikana amekana tuhuma za kulala nyumba ya wageni na kufanya tendo la ndoa na muumini huyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments