MWANDISHI WA ITV AUAWA NA KUTUPWA NJIA PANDA

Jeshi la Polisi mkoa wa Kipolisi Kinondoni limethibitisha kutupwa kwa mwili wa aliyekuwa mwandishi wa habari ITV/Radio one na mtayarishaji wa kipindi cha Jarida la Wanawake, Blandina Sembu katika eneo la njia panda ya ITV na watu wasiojulikana waliokuwa wakitumia gari aina ya Noah.

Pia Kituo cha Runinga cha ITV kimeripoti taarifa za uthibitisho kuhusu kupatikana kwa mwili wa Blandina Sembu ukiwa umetupwa njia panda ya ITV, Mwenge mkoani Dar es salaam.


Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Polisi Kinondoni
hadi sasa watu waliofanya hivyo hawajajulikana na msako unaendelea.


CHANZO - DIRAMAKINI BLOG

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post