
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaeleza kuwa mwili wa mwenyekiti huyo wa chama cha ACT-Wazalendo aliyefariki dunia leo saa 5 asubuhi katika hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) utaondoka na ndege kesho asubuhi kwenda mjini Unguja ambako itafanyika sala katika viwanja wa Mnazi Mmoja.
Inaeleza kuwa saa 6 mchana utasafirishwa kwenda Pemba na sala itafanyika katika viwanja vya Gombani na kisha safari ya kueleka Mtambwe kwa mazishi yatakayofanyika saa 10 jioni itaanza.
Social Plugin