Picha : MWILI WA MAALIM SEIF SHARIF HAMAD UKIWASILI UWANJA WA NDEGE WA ZANZIBAR


Mwili wa Marehemu aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad ukishushwa katika Helikota ya JWTZ baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar ukitokea Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Zanzibar a na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhajj Dk. Hussein Aliu Mwinyi na (kushoto)Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe.Hemed Suleimn Andulla na (kulia) Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magjaribi Unguja Mhe.Idreisa Kitwana Mustafa na Viongozi wengi wa Serikali na Chama wakiupokea Mwili wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, ulipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amari Karume Jijini Zanzibar, kwa ajili ya kuangwa na Wananchi wa Zanzibar katika viwanja vya Mnazi mmoja na kusafirika kwenda Pemba kwa maziko leo jioni.


Wananchi wa Zanzibar wakiwa katika viwanja vya Mnazi mmoja wakisubiri kusalia mwili wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad,katika viwanja hivyo kabla ya kusafirishwa kwenda Pemba kwa maziko.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments