SERIKALI YAKAMILISHA UJENZI WA KITUO CHA KUPOZEA UMEME WA SGR
Sunday, January 31, 2021
Serikali kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limekamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme itakayotumika kuendesha treni ya mwendokasi (SGR) kutoka jijini Dar es Salaam hadi mkoani Morogoro huku awamu ya pili kutoka mkoani Morogoro kuelekea Matukupola mkoani Dodoma ikitarajiwa kuanza hivi karibuni.
Akizungumza mjini Morogoro mara baada ya kutembelea kituo cha kupozea umeme kilichopo Kingolwira nje kidogo ya Manispaa ya Morogoro, Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amesema kwa sasa ujenzi wa miundombinu hiyo yenye urefu wa kilomita 160 imekamilika kwa asilimia 100.
Kwa upande wake Meneja Mwandamizi wa miradi kutoka TANESCO, Mhandisi Emmanuel Manilabona amesema vituo vyote vya kupoza umeme vilivyopo katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro tayari vimeshakalimika.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin