HATIMAYE MAMA DANGOTE AMTAJA BABA MZAZI WA MSANII DIAMOND PLATNUMZ


Sanura Kassim maarufu mama Dangote ambaye ni mama mzazi wa msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz amesema baba halisi wa mwanaye ni Salum Iddi Nyange na si Abdul Juma ambaye kwa miaka mingi amekuwa akifahamika kama baba wa mkali huyo wa Bongofleva.

Mama Dangote ameeleza hayo leo Ijumaa Januari 15, 2021 baada ya kupigiwa simu na Dida, mtangazaji wa kipindi cha Mashamsham kinachorushwa na redio ya Wasafi kueleza kuhusu uhusiano kati ya Diamond na Ricardo Momo aliyekuwa akihojiwa na redio hiyo.

Katika majibu yake, mama Dangote amesema Ricardo na Diamond ni ndugu na baba yao ni Nyange ambaye kwa sasa ni marehemu.

Chanzo - Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments