Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba (kulia), kushoto ni mfano wa kinu na mtwangio
Na Kadama
Malunde – Malunde 1 blog
Mwanamke aitwaye Paulina Daudi (30) mkazi wa Mtaa wa Mageuzi kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga ameuawa kwa kupigwa ngumi na mchi wa kinu ‘mtwangio’ na mmewe aitwaye Samwel James baada ya kutokea ugomvi wa kifamilia.
Kwa Mujibu
wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba tukio hilo
limetokeo Jumanne Januari 26,2021 majira ya saa tatu asubuhi na kutaja chanzo
cha mauaji hayo kuwa ni ugomvi wa kifamilia.
“Paulina Daudi (30) mkazi wa Mageuzi alishambuliwa kwa
kupigwa ngumi na mchi mdogo ‘mtwangio’ sehemu mbalimbali za mwili wake na mume
wake aitwaye Samwel James akiwa nyumbani”,amesema
Kamanda Magiligimba.
Ameeleza
kuwa Paulina Daudi alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya
Rufaa mkoa wa Shinyanga.
Ameongeza
kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na juhudi za kumtafuta na kumkamata mtuhumiwa
Samwel James kwa kosa la mauaji kwani alikimbia mara baada ya tukio hilo.
Kamanda
Magiligimba anatoa wito kwa wanandoa kuacha mara moja tabia ya kuwashambulia
wenza wao.
Aidha amewasisitiza wanawake wote wanaofanyiwa
vitendo vya ukatili mkoani shinyanga
wavunje ukimya,wafunguke ili matatizo yao ya kifamilia yaweze
kushugulikiwa yakiwa katika hatua za
awali kabla madhara makubwa hayajatokea akibainisha kuwa vitendo vya ukatili ni uhalifu kama ulivyo uhalifu mwingine.
Social Plugin