RAIS WA MSUMBIJI NYUSI ATUA TANZANIA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI KANDA YA CHATO



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshuhudia mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi akimwagilia maji mti alioupanda baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi zawadi ya picha ya kuchora ya THE BIG FIVE mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi katika Ikulu ndogo ya Chato mkoani Geita baada ya kuwasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakimsikiliza Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto baada ya kuweka Jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita alikowasili kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakisikiliza maelezo toka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto kabla ya kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Januari 11, 2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimtambulisha kwa viongozi mbalimbali mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi alipowasili ili kuweka jiwe la Msingi la Ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Chato mkoani Geita leo Jumatatu Januari 11, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakifurahia ngoma za utamaduni katika Uwanja wa Ndege wa Geita mara alipowasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku moja leo Jumatatu Januari 11, 2021

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments