SPIKA NDUGAI AWAAPISHA WABUNGE WATEULE WA RAIS MAGUFULI
Wednesday, December 09, 2020
Spika wa Bunge Job Ndugai, amewaapisha Dkt Dorothy Gwajima na Dkt Leonard Chamuriho kuwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wabunge hao wameapishwa kufuatia kuteuliwa na Rais John Magufuli hivi karibuni na kisha kupewa nyadhifa za Uwaziri katika Baraza jipya la Mawaziri alilolitangaza.
Hafla ya kuwaapisha Wabunge hao wawili imefanyika jijini Dodoma na kuhudhuriwa na watu mbalimbali.
Dkt Dorothy Gwajima ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) anayeshughulikia Afya ameteuliwa kuwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Dkt Leonard Chamuriho aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Uchukuzi ameteuliwa na Rais Magufuli kuwa Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin