MADIWANI WA VITI MAALUMU 64 MKOANI KAGERA WAPATIWA ELIMU YA LISHE BORA

Mhe Neema Lugangira (Mb.) ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shirika la Agri Thamani akitoa Mafunzo ya Lishe Bora kwa Madiwani Viti Maalum
Mwenyekiti wa UWT Mkoa Hajat Faiza kulia akichukua dondoo kwenye  Mafunzo ya Lishe Bora na Madiwani Viti Maalum wa Mkoa wa Kagera
Mhe Hajat Mwajabu Mhe Naibu Mstahiki Meya wa Bukoba Manispaa wa pili kutoka kushoto  akiandika mambo anayokwenda kufanyia kazi baada ya Mafunzo ya Lishe Bora

MADIWANI wa Viti Maalumu wapatao 64 kutoka Mkoani Kagera wamepatiwa mafunzo ya Lishe Bora kuhusu umuhimu wake na madhara yake ikiwemo ya kiuchumi iwapo hawatazingatia .

Mafunzo hayo yametolewa na Shirika la Agri Thamani yakiwa na lengo la kuwaelimisha kwa kina madiwani hao wanawake kuhusu umuhimu wa lishe bora kwa mama mjamzito, mama anaenyonyesha, mtoto chini ya miaka 5, kijana balehe, wanaume na wazee n.k.
 
 Aidha madiwani hao pia walipata uelewa pia juu ya hali ya lishe nchini, madhara yake katika uzalishaji, jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali, malengo ya Chama Cha Mapinduzi kupitia Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 na wajibu wao kama viongozi.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Mkurugenzi wa Shirika la Agri Thamani, Mhe Neema Lugangira (Mb) alisema kwamba baada ya mafunzo hayo wanategemea kuona bajeti ya lishe ikiongezwa na kutolewa.

Alisema bajeti hiyo itakapotolewa itumike kwa ajili ya afua za lishe zinazokubalika na hilo linawezekana sababu Madiwani Viti Maalumu wanashiriki vikao vinavyopitisha bajeti za Halmashauri na hivyo itakuwa rahisi kwao kuweza kuitetea na kuifuatilia. 

Kwa upande wao Madiwani waliazimia kuanza na ajenda kuu tano ambazo ni kujua hali za lishe za wilaya zao, utengaji wa bajeti ya lishe, kujua aina za afua za lishe zinazokubalika, utendaji wa kamati za lishe na utekelezaji wa mikataba ya lishe iliyosainiwa kati ya Mkuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya zao.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments