Mabadiliko Ya Manaibu Makamishna Wa Uhifadhi Wawili Wa Mamlaka Ya Hifadhi Ya Ngorongoro
Sunday, December 20, 2020
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Damas D. Ndumbaro (Mb), kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa Sheria ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Sura Na. 284, tarehe 19 Disemba, 2020 amefanya mabadiliko ya Manaibu Makamishna wa Uhifadhi wawili wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), kwa lengo la kuboresha utendaji kazi wa Taasisi hii.
Katika mabadiliko hayo, Mhe Waziri amemteua Dkt. Christopher D. Timbuka, kuwa Kaimu Naibu Kamishna (Uhifadhi, Utalii na Maendeleo ya Jamii). Kabla ya uteuzi huo, Dkt. Timbuka alikuwa Kamishna Mwandamizi wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA), Kanda ya Kusini. Anachukua nafasi ya Bw. Ephraim A. Mwangomo ambaye amerejeshwa TANAPA.
Aidha, Mhe Waziri amemteua Bw. Audax R. Bahweitima, kuwa Kaimu Naibu Kamishna wa Uhifadhi (Huduma za Shirika). Kabla ya uteuzi huo, Bw. Bahweitima alikuwa Mchumi Mkuu katika Idara ya Sera na Mipango, Wizara ya Maliasili na Utalii. Anachukua nafasi ya Bw. Abdallah O. Kiwango ambaye amerejeshwa TANAPA.
Uteuzi huo unaanza rasmi tarehe 19 Disemba, 2020.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin