KANISA LA ABC LAWAKUMBUKA WAJANE, WAGANE NA WATOTO KRISMASI

 

Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila (katikati) akikabidhi juzi msaada wa chakula na vitu vingine kwa Wagane na Wajane.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila akikabidhi juzi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto wenye uhitaji.Kulia ni mke wake Janeth Ndabila.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila akikabidhi juzi msaada wa vifaa vya shule kwa watoto wenye uhitaji.Kulia ni Mke wake Janeth Ndabila.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila akikabidhi juzi msaada wa chakula kwa Nasaba  Seifu.
Mgane Hussein Libe akishukuru baada ya kupokea msaada huo.
Mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Mandela, Leonard  Chalema na Tabrisa Bushiri 
Wajane wakiondoka katika kanisa hilo baada ya kupokea msaada huo.
Mjumbe wa Serikali ya mtaa wa Mandela, Leonard  Chalema akizungumza baada ya kupokea msaada huo.
Wajane wakiwa katika kanisa hilo wakati wakisubiri kupokea msaada wa chakula.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila, akizungumza na Wajane kabla ya kuwakabidhi msaada huo.
Askofu Kiongozi wa Kanisa la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam, Flaston Ndabila (wa pili kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mtaa wa Tabata Mandela na watoto wenye uhitaji baada ya kuwakabidhi juzi msaada wa vifaa vya shule
 

Na Dotto Mwaibale.

KANISA la Abundant Blessing Centre (ABC) la Mtaa wa Mandela jijini Dar es Salaam limetoa msaada wa chakula na vitu vingine kwa ajili ya kuwasaidia Wagane na Wajane 50 wanaoishi kwenye mtaa huo.

Mbali na kutoa msaada pia kanisa hilo limetoa msaada wa vifaa vya shuleni kama madaftari na kalamu kwa watoto 20 wenye uhitaji ikiwa ni maandalizi ya masomo watakayoanza Januari 2021.

Akizungumza juzi wakati wa kukabidhi msaada huo Askofu Kiongozi wa kanisa hilo Flaston  Ndabila alisema wamekuwa wakiguswa na changamoto mbalimbali za Wajane na wagane pamoja na wanafunzi wanaoishi mtaa huo na ndio maana  kama kanisa wameweka utaratibu kila mwaka kutoa msaada huo.

"Huu ni mwaka wetu wa tano tumekuwa tukifanya hivi  hasa kipindi hiki cha Sikukuu za mwishoni mwa mwaka za Krismas na mwaka mpya kuelekea mwezi wa kwanza ambapo watoto hawa wenye uhitaji wanakuwa wanakabiliwa na changamoto ya vifaa vya shule" alisema Ndabila. 

Aidha Ndabila alisema wanatoa msaada huo kwa wanafunzi hao ikiwa ni kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt.John Magufuli ambayo inatoa elimu bure kuanzia shule ya msingi hadi sekondari. 

Wajumbe wa Serikali ya mtaa wa Mandela, Leonard  Chalema na Tabrisa Bushiri kwa niaba ya Mwenyekiti wa mtaa huo, Yusufu  Nyumbi wakipokea msaada huo wamelishukuru kanisa hilo kwa utaratibu wao wa kila mwaka wa kuwajali wenye uhitaji.

Mgane Hussein Libe ambaye huu ni  mwaka wake  wa tatu kupata msaada huo alisema kanisa hilo ni mfano wa kuigwa na akashauri makanisa mengine kuiga mfano huo wa kusaidia jamii badala ya kuiachia Serikali pekee kufanya hivyo. 

Hosiana Mkono ambaye ni mjane amelishukuru kanisa hilo kwa kutoa msaada huo na kugusa maisha ya wenye uhitaji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments