MAGUFULI: VITAMBULISHO VYA WAJASIRIAMALI VITABORESHWA


Rais Magufuli   amesema, vitambulisho vya wajasiriamali ‘machinga’ vitaboreshwa zaidi ili kuwawezesha kupata mikopo benki.

Rais Magufuli amesema hayo wakati akihutubia na kuzindua Bunge la 12 leo Ijumaa tarehe 13 Novemba 2020 jijini Dodoma.
 

Amesema, katika kipindi cha miaka mitano ijayo, vitambulisho vya wajasirimali vilivyokuwa vinatolewa huko nyuma sasa vitaboreshwa zaidi kwa kuweka taarifa muhimu.

“Kwa miaka mitano ijayo, tutaviboresha ikiwemo kuweka picha na taarifa nyingine muhimu kama ilivyo kwenye vitambulisho vya taifa na paspoti.

“Hii itawezesha wafanyabiashara watakaotumia vitambulisho hivyo kutambulika ikiwemo kwenye benki na hivyo kupata mikopo ili kukuza biashara zao,” amesema Rais Magufuli

Amesema, hatua hiyo “itawawezesha kukuwa na kutajirika, tunataka wafanyabiashara wadogo wadogo kukuwa na siyo kubaki walivyo”



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments