IDARA YA UTAMADUNI YAAGIZWA KUFANYA MAANDALIZI YA UZINDUZI WA BODI YA MFUKO WA UTAMADUNI NA SANAA

 Na Shamimu Nyaki – WHUSM, Dodoma
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt.Hassan Abbasi ameiagiza Idara ya Maendeleo ya Utamaduni ya Wizara hiyo kuanza maandalizi ya kuzindua Bodi ya Mfuko wa Utamaduni na Sanaa.

Katibu Mkuu Dkt.Abbasi ametoa maagizo hayo Novemba 24, Jijini Dodoma katika kikao chake na Idara hiyo.

Dkt.Abbasi ameiagiza Idara hiyo kusimamia vyema Taasisi zilizo chini yake hasa inayohusika na kukuza na kuendeleza Lugha ya Kiswahili ndani na nje ya nchi.

Aidha, Dkt. Abbasi ameitaka Idara hiyo kuratibu matamasha mbalimbali huku akieleza nia ya kuwa na tamasha la Singeli Festival mwishoni mwa mwezi Desemba, 2020.

MWISHO.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments