MCHEZA MIELEKA MAARUFU UNDERTAKER AJIUZULU WWE



Mchezaji maarufu wa mchezo wa mieleka- Undertaker 

Mchezaji maarufu wa mchezo wa mieleka- Undertaker amethibitisha rasmi kujiuzulu kutoka WWE baada ya miaka 30.

Aliingia ulingoni kwa mchezo wa mwisho katika mchezo wa mwisho wa Survivor Series Jumapili usiku, ambapo aliuhutubia umma wa mashabiki wa WWE Universe kwa mara ya mwisho.

Wakati wa hotuba yake, Undertaker ambaye jina lake halisi ni Mark Calaway –alieleza ni kwanini ameamua kujiuzulu.

"Kwa miaka 30 nimekuwa nikiingia ndani ya ulingo huu taratibu na kuwaangusha watu mara kwa mara," alisema.

"Sasa wangu muda umefika. Muda wangu umefika wa kumuacha Undertaker apumzike... kwa ... amani."

Calaway anajiuzulu akiwa ndiye mchezaji bora wa WWE kuwahi kushuhudiwa katika mashindano hayo na amekuwa ulingoni kwa miongo mitatu na atakumbukwa na mashapiki wake daima.

Chanzo - BBC

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments