MWALIMU AKAMATWA KWA KUMBAKA CHOONI MWANAFUNZI WAKE WA DARASA LA TANO











Kamanda wa Polisi, mkoa wa Morogoro, SACP Wilbroad Mutafungwa.

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro, linamshikilia mwalimu wa taaluma katika Shule ya Msingi Montfort, Eneza Andarson, 27, kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 10, kwa nyakati tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro, SACP Wilbroad Mutafungwa, amesema kuwa mtuhumiwa huyo amekuwa akifanya kitendo hicho cha unyanyasaji kwa mwanafunzi huyo mara kwa mara katika maeneo mbalimbali shuleni hapo, ikiwemo ofisini na hata kumfuata chooni.

"Mwanafunzi huyo ni mkazi wa Kihonda baada ya kumhoji alikubali kufanyiwa vitendo hivyo na mwalimu wake na aliweza kusimulia namna ambavyo alikuwa anafanyiwa vitendo hivyo vya kikatili, wakati mwingine alikuwa anafanyiwa chooni na hata ofisini", ameeleza Kamanda Mutafungwa.

Aidha Kamanda Mutafungwa, amewashauri wazazi kuhakikisha wanafuatilia mienendo ya watoto wao , ikiwemo kuwakagua ili kujihakikisha kama hakuna vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa.

CHANZO- EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments