ZEC YAMFUNGIA MAALIM SEIF KUFANYA KAMPENI KWA SIKU 5
Friday, October 16, 2020
Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imemsimamisha mgombea Urais wa Zanzibar kupitia chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad kutofanya mikutano ya kampeni za Urais kwa siku 5 baada ya kuonekana na kosa la uvunjifu wa maadili.
Akitangaza maamuzi ya Kamati ya maadili ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar Katibu wa Kamati hiyo ya Maadili Khamis Issa Khamis amesema tume ilipokea malalmiko kutoka kwa mgombea wa Urais wa chama cha Demokrasia Makini Ameir Hassan Ameir dhidi ya mgombea Maalim Seif ya kuhamasisha wananchama wake wakapige kura siku ya kura ya awali.
Katibu wa kamati amesema kamati ilisikiliza hoja zote na kuona kuwa mgombea Maalim Seif ametenda kosa hilo na kumpa adhabu kwa mujibu wa sheria kifungu cha 23 D za kanuni za maadili.
Kamati hiyo ya maadili imetoa fursa kwa Maliam Seif kukata rufaa endapo haajridhika na mammzui hayo
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin