YALIYOJIRI KATIKA ZIARA YA KITAIFA YA RAIS WA MALAWI MHE. DKT. LAZARUS MCCARTHY CHAKWERA TANZANIA

Tanzania na Malawi zimekubaliana kushirikiana kuboresha sekta za usafirishaji, uvuvi, madini, nishati, utalii na kilimo.
Makubaliano hayo yalitangazwa jana Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa hafla maalum iliyohusisha marais wa nchi hizo mbili, mwenyeji Dk. John Magufuli na Rais Lazarus Chakwera aliyezuru nchini kwa ziara ya siku tatu.

Rais Magufuli alimshukuru Rais Chakwera kwa kuitembelea Tanzania na kuwa nchi ya tatu kutembelewa barani Afrika kwa kiongozi mpya wa Malawi baada ya Burundi na Uganda tangu aingie madarakani.

Katika hafla hiyo, Rais Magufuli alisema nchi hizo mbili zina historia ya undugu kutokana na mwingiliano wa watu wake katika shughuli mbalimbali ikiwamo biashara.

 



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments