IGP SIRRO AONYA VIKUNDI VILIVYOPANGA KUFANYA VURUGU ARUSHA


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro amesema jeshi lake limepata taarifa za kuwepo kwa baadhi ya vikundi vichache katika Jiji la Arusha vyenye nia ya kuharibu amani siku ya uchaguzi na kutoa onyo kali kwa wote wenye mpango huo.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo Jijini Arusha baada ya kuzungumza na askari polisi zaidi ya 700 watakaosimamia mchakato wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika nchini kote siku ya Jumatano Oktoba 28,2020.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi pia ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wa Mkoa wa Arusha kuendelea kuimarsha amani na utulivu siku hiyo ya uchaguzi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments