Picha : LORI LA MAFUTA LAWAKA MOTO MOROGORO

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Morogoro limefanikiwa kuudhibiti moto wa mafuta kutokana na gari lenye namba za usajili T862 BZS na tela namba T814 DBZ kushika moto katika eneo la Kiegea, Wilayani Kilosa.



Kwa mujibu wa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto (SACF), Goodluck Zelote amesema hakukuwa na madhara yoyote kwa binadamu na chanzo cha moto huo hakikujulikana mara moja ila inasadikika ni hitilafu katika mfumo wa umeme wa gari hilo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527